Jabhat Al Nusrah yaahidi kusimika Imara ya Kislaam kwenye Ardhi ya Syria.

Sunday July 13, 2014 - 15:41:21
8217
Super Admin
Uongozi wa Jabhat Al Nusrah unaopigana nchini Syria umetangaza kuunda Imara ya Kislaam itakayofanyakazi yake kwenye Ardhi ya Shaam.




Baada ya kurikodiwa sauti ya siri kiongozi wa Jabhat Al Nusra Sheikh Mohamed Jowlaani alisema kuwa Jabhat Al Nusra itaunda Imara ya Kislaam kwenye Ardhi ya Shaam na kundi hilo tayari limethibitisha taarifa hiyo.





Taarifa rasmi iliyotolewa na kusambazwa kwenye ukurasa wake wa Tiwtter Kundi la Kislaam la Jabhat Al Nusra limesema uongozi wa Kundi hilo linafanya kila liwezekanalo kuweka mfumo wa Sheria za Kislaam katika nchi ya Syria.




"Lengo la Jabhat Al Nusra tangu kuanzishwa kwake ni kuitwabiqisha Sheria za Allah katika nchi ya Syria"ilisema sehemu ya taarif hiyo iliyotolewa na Al Nusrah.




Al Nusra imewaonya Makundi ya Ki'almaani inayoendesha miradi dhidi ya Nidhamu ya Sheria za Kislaam nchini Syria.




Mwisho kabisa Jabhat Al Nusrah imetangaza kuendelea na Mapigano dhidi ya Utawala wa Kinuseyria wa Bashar Al Asad na kile ilichokiita Makundi ya Ki Khawaariji Ghullaad inayoilenga Dola ya Kislaam ambayo miezi ya hivi karibuni iliuchukua Mikoa ya Hasaakah na Deyrazuur zilizo na utajiri wa Mafuta.

Related Items

Update cookies preferences