UFAFANUZI:Maaskari na Maofisa wa Uganda waliouawa kwenye shambulio uliofanyika Mkoa wa Lower Shabelle.

Friday July 18, 2014 - 01:36:01
8876
Super Admin
Kumepatikana habari zaidi kuhusiana na mlipuko uliofanyika jana jioni katika mkoa wa Lower Shabelle ambapo ulilengwa kambi ya Wanajeshi wa Kigeni.






Duru za kuaminika iliyopatikana Lower Shabelle ilieleza kuwa Wanajeshi 5 kutoka Uganda wameuawa kwenye Mlipuko mkubwa uliolengwa Kituo cha Wanajeshi wa AMISOM huko wanajeshi zaidi ya 10 wakijeruhiwa vibaya na pia Maofisa watatu wa Kijeshi waliokuwa wakiongoza Mapigano wameuawa kwenye mkasa huo ambao ulitokana na Gari iliyokuwa imejazwa vitu vya vilipuzi.





Habari zaidi zinaeleza Magari ya kijeshi ya Wanajeshi wa AMISOM yaliokuwa eneo la mlipuko nazo ziliteketea na kuharibiwa vibaya,Mashuhuda wanasema waliona moshi mkubwa uliokuwa umetanda angani.




Mpaka sasa hakuna taarifa rasmi kutoka upande wa uongozi wa AMISOM kuhusiana na Mlipuko huo uliosababisha vifo vya Wanajeshi wao na Magari yao kuteketea kutokana na shambulio hilo.




Mahad Yare


SomaliMem,Mugadishu


Related Items

Update cookies preferences