Afisa mmoja mwenye cheo cha juu wa Serikali ya FG auawa mjini Mugadishu na mlipuko uliofanyika Wilaya ya Hodhan.

Friday July 18, 2014 - 01:39:23
6515
Super Admin
Watu waliojihami na Silaha wamemwua kwa kumpiga risasi Afisa mwenye cheo cha juu kwenye jeshi la Polisi la Serikali Shirikisho la Somalia FG katika Wilaya ya Wadajir mjini Mugadishu.



Walioshuhudia wanasema watu waliokuwa na silaha za Pisto katika mtaa wa Korontada Wilayani Wadajir walimtwanga risasi Afisa aliyekuwa na cheo cha Col, katika jeshi la Polisi la Serikali ya FG.




Upande mwingine kulitokea mlipuko mkubwa katika eneo la Hospitali ya Digfeer Wilayani Hodan ambapo walilengwa Gari waliokuwemo Maofisa wa Jeshi la Polisi wa Serikali ya FG.




Habari za awali zinaeleza kuwa Afisa aliyelengwa Shambulio hilo la Bomu ameuawa na Bomu hilo huko 3 miongoni mwa maofisa hao waliokuwemo kwenye Gari iliyolengwa wakijeruhiwa vibaya.

Related Items

Update cookies preferences