Kwenye kipindi cha malumbano ya hoja unaoendeshwa na Televisheni ya kiarabu ya Al-Jazeera iliyo na makao yake nchini Qatar leo imegeuka na kuwa ulingo wa kucheza michezo wa Ndondi baada ya wachambuzi wawili kutoka upande wa Waislaam wa Kisunni na Kishia kuanza kuchapana kabla hawajaamuliwa.
Kama ilivyo kawaida kwenye kipindi hicho inayoendeshwa na mtangazaji mashuhuri wa televisheni ya Al-Jazeera Dr. Feysal Al Qasim hukutanishwa watu wawili walio na rai tofauti zinazopingana,na wiki hii ilikuwa hoja inayohusiana na hali nchini Iraq.
Na Kwenye Studio hiyo walikutanishwa watu wawili kutoka upande wa Waislaam wa Kisunni na Kishia,na mmoja wao alikuwa akiitetea nidhamu ya kishia wa Nuri Al Maliki,huko mwingine akiitetea VuguVugu uliojihami nchini Iraq,na mwishowe wawili hao kuamua kuanza kuchapana kabla haawjazuiwa na Walinzi wa Studio ya Al Jazeera.
TIZAMA VIDEO HAPA CHINI