Serikali ya Canada imetangaza kuwa mtoto wa aliyewahi kuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya TFG amejiunga na Mujahidina nchini Syria.
Faarah Mohamed Faarah Shirdoon ambae alikuwa miongoni mwa Jamii ya Wasomali waishio nchini Canada khususan mji wa Calgary alionekana kwenye Video ya kidokmentari iliyosambazwa na Dola ya Kislaam ya Iraq na Shaam akichana chana hati yake ya kusafiria.
Mtandao wa CBC News la nchini Canada ilizuru nyumba alikukuwa akiishi kwenye mji wa Calagary Faarah Mohamed Faarah Shirdoon na ilifanya mahojiano na familia na jamaa zake Faarah na kusema kuwa walishtushwa baada ya kumwona kwenye vyombo vya habari akichanachana hati yake ya kusafiria ya Canada.
Familia ya Faarah ni maarufu nchini Canada na ni familia walioingia kwenye ulingo za siasa nchini Somalia lakini mtoto wao alikuwa na maono tofauti na kupenda kushiriki Jihadi inayoendelea Dunia ya Kislaam.
Mujahidi huyo wa Kisomali ambae humwita baba mdogo aliyewahi kuwa Waziri mkuu nchini Somalia Abdi Faarah Shirdoon mwaka 2012 alihitimu na kumaliza Chuo kikuu cha Alberta Institute of Technology na Jamii ya Kisomali waishio nchini Canada walikiri kuwa Faarah alikuwa ni msomi aliyefika kiwango cha juu katika masuala ya Teknoljia ya Kisasa.
Kitengo cha habari na matangazo cha Al Furqaan iliyo chini ya Dola ya Kislaam ya Iraq na Shaam miezi miwili iliyopita ilitangaza Video iliyomwonyesha Faarah akichana chana hati yake ya kusafiria na kuionya Serikali ya Canada na Marekani.
Michel Coulombe ambae ni mkuu wa kitengo cha upelelezi nchini Canada alisema mwezi February mwaka huu kuwa vijana wa kislaam wapato 130 walisafiri kwenda nchi za Syria,Yemen,Somalia na kaskazini mwa Bara la Afrika.
Liban Jehow Abdi
SomaliMemo,Mugadishu