Al Nadif atangaza kujiuzulu na mgongano wa kisiasa uliopo baina ya Mataifa yalioungana kwa jina la AMISOM.

Friday June 20, 2014 - 20:33:37
10725
Super Admin
Aliyekuwa mwakilishi wa Somalia kwa A.U Mohamed Saleh Al Nadif.
Aliyekuwa mwakilishi wa Somalia kwa A.U Mohamed Saleh Al Nadif.
Mohamed Salah Al Nadif mwakilishi maalumu wa masuala ya Somalia kwa upande wa Umoja wa Afrika ametangaza amejiuzulu kwenye nyadhifa wake aliyokuwa nayo kwenye umoja huo.




Taarifa rasmi uliotolewa na Al Nadif mwenyewe ilithibitisha kujiuzulu kwake takriban miaka miwili sasa lakini sababu ya kujiuzulu kwa Afisa huyo ahaikutajwa.





Vyanzo vya kuaminika vinaarifu kuwa mgongano mkubwa wa kiasiasa uliopo baina ya mataifa yalioungana kupeleka Wanajeshi wao nchini Somalia ndio inaaminika chanzo cha kuachia ngazi kwa Afisa huyo wa African Union.





Afisa huyo aliyetangaza kujiuzulu katika miezi ya hivi karibuni alikuwa akipigania kuwa Wanajeshi wavamizi kutoka nchini Kenya waliopo mji wa Kismaayo kuondolewa na badala yake kupelekwa Wanajeshi wa Burundi na Siaralione hatua iliyopingwa na Serikali ya Kenya na Uganda.





Al Nadif na Rais wa Djibuti pamoja na Kiongozi wa Serikali ya TFG Hassan Sheikh kwa upande wa kisiasa wako karibu zaidi,Duru za kuaminika zinaeleza kuwa baadhi ya Viongozi wengine wa AMISOM wanapanga nao kujiuzulu.





Msemaji wa AMISOM Col.Ali Hamuud ambae ni Mjibuti amesema katika mazungumzo yake ya mwisho kabisa kuwahi kutoa kuwa Serikali ya Djibuti haijafurahishwa na mwenendo mzima wa Wanajeshi wa AMISOM walioivamia Somalia khususan idadi ya Wanajeshi 400 kutoka Uganda waliopelekwa mjini Mugadishu kwajili ya kulinda Ofisi za Umoja wa Mataifa.




Mataifa Vibaraka wa Afrika walioivamia Ardhi ya Somalia kila mwezi hupokea mamilioni ya Dola za Kimarekani ambao unafadhiliwa na Amerika na Umoja wa nchi za Ulaya na unasubiriwa mwisho wa Mradi huu na hatima ya Mataifa hayo ya Kiafrika baada ya kutumiwa na Mataifa hayo makubwa.





Mataifa hayo ya Kiafrika yaliofanya Uvamizi katika Ardhi ya Somalia yana maono tofauti na fikra za mbali lakini chanzo cha yote ni Ruzuku hiyo inayotoka kwa Amerika na Washirika wake pamoja na Vita vyao dhidi ya Sheria za Kislaam nchini Somalia.




Mohamed Saleh Al Nadif ni mzaliwa wa nchi ya Chad huko akiwa tayari ameshawahi kufanyakazi katika Wizara ya Masuala ya nje wa nchi hiyo.




Kwenye miji yaliowekwa Mzingiro na Vikosi vya Harakat Al-Shabab Al Mujahideen ni mmoja wapo ya changamoto kadhaa iliyomkabili Al Nadif alipokuwa kwenye cheo chake nchini Somalia.




Liban Jehow Abdi



SomaliMemo,Mugadishu



Related Items

Update cookies preferences