Col.Hassan Dahir na Maofisa wa Ujususi wa Serikali ya FG wauawa mjini Mugadishu

Wednesday July 09, 2014 - 10:43:45
7933
Super Admin
Wakati ambapo hali ya usalama ukiwa tete mjini Mugadishu mauaji ya kupangwa yameendela kufanyika kwa mara nyingine jana usiku katika mitaa mbalimbali mjini humo.



Watu waliojihami na silaha walimpiga risasi Afisa mmoja wa Ujasusi wa Serikali ya FG kwenye eneo la makutano ya Barabara ya KPP Wilayani Hodon mjini Mugadishu.




Vyanzo vya habari vimedokeza kuwa ameuawa Afisa aliyekuwa akijuikana kwa jina la Col.Hassan Dahir ambao alishawahi kuwa Mkuu wa Gereza la IKULU lakini miezi michache iliyopita aliondolewa cheo hicho.




Walioshuhudia wanasema Col.Hassan Dahir aliuawa pamoja na Askari aliyekuwa nayo,upande mwingine Afisa mwingine wa Serikali ameuawa mtaa wa Howl Wadaag mjini Mugadishu.




Shambulio lingine iliyofanyika Wilaya ya Huriwaa nako wameuawa Maofisa wawili wa Jeshi la Serikali ya FG,upande mwingine kulisikika uftyatulianaji wa Risasi katikati mwa mji wa Mugadishu wakati ambapo shambulio la IKULU ukiendelea jana usiku.

Related Items

Update cookies preferences