Wahusika wa Mauaji ya Masheikh Aboud Rogo,Samir Khan hawajakamatwa,Polisi nchini Kenya "Tumemkamata mtuhumiwa wa mauaji ya Sheikh Mohamed Idrisa!"

Friday June 20, 2014 - 11:07:32
30373
Al Akh Mohamed Sudi Mohamed aliyedhulumiwa na Polisi nchini Kenya.
Al Akh Mohamed Sudi Mohamed aliyedhulumiwa na Polisi nchini Kenya.
Katika hali ya kushangaza Polisi wa kupambana na Uislaam nchini Kenya wametangaza kumkamata waliyemtaja kuwa ni mtuhumiwa wa mauaji ya Sheikh Mohamed Idrisa na huko wakimsingizia kuwa alikuwa akimiliki silaha kinyume na Sheria.



Waislaam wanajiuliza hivi kwanini Serikali ya Kenya haijawakamata walio nyuma ya mauaji ya Mashekhe kadhaa waliouawa mjini Mombasa na mji wa Garissa na badala yake inawakata wasio husika na mauaji ya Sheikh Mohamed Idrisa aliyekuwa ngao kwa Serikali ya Kenya.





Hii ni Ishara ya Wazi kuwa Serikali ya Kenya kwa kushirikiana na Amerika inao Baadhi ya viongozi wa Kislaam wanaojiita mashekhe ambao wanatetea maslahi ya Serikali hiyo iliyomwaga Damu ya Wasilaam nchini Kenya.




Gazeti la The Standard la Kenya iliarifu kuwa Maofisa wa Kupambana na Uislaam nchini Kenya wamekamatwa mtu waliyemtaja kuwa mtuhumiwa wa mauaji ya Sheikh Mohamed Idrisa aliyeuawa mjini Mombasa siku chache zilizopita.




Polisi wanasema Mohamed Sudi Mohamed ndie mtumhimwa wa Mauaji ya Sheikh Mohamed Idrisa,Mohamed Sudi alikamatwa mtaa wa Likoni mjini Mombasa na kuongeza kuwa Mohamed Sudi alikuwa akimiliki Silaha nyumbani kwake pamoja na vifaa vya vilipuzi bila ya kuonyesha ushaidi kama ilivyokawaida ya Polisi hao wa Kenya.




Mohamed Sudi Mohamed Kesi yake imeakharishwa hadi tarehe 30 june mwaka huu ambapo ambapo alikana tuhuma zote aliyosingiziwa na Polisi wa kupambana na Uislaam nchini Kenya.

Related Items

Update cookies preferences