Habari kutoka mikoa ya Lower Jubba zinaeleza kuwa kumekuwa na makabiliano makali yaliodumu masaa kadhaa katika Maeneo ya miji ya Kulibiyow na Badade karibu na mipaka ya kizushi kati ya nchi hizi mbili ya Somalia na Kenya.
Vyanzo
vya kuaminika vinaeleza kuwa Mujahidina wa Wilayatul Islamiah ya Lower
Jubba walifanya shambulio la kushtukisha dhidi ya Msafara wa Wanajeshi
waliokuwa wakitembe eneo la mpaka ambapo mapigano yalidumu takriban
masaa matatu mfululizo.
Waandishi wa
habari waliopo mkoa wa Jubba wanasema Magari 4 ya Wanajeshi wa Kenya
zimeteketezwa na Wanajeshi waliouawa ni zaidi ya Wanajeshi 10.
Habari
zaidi zinaeleza kuwa kati ya Magari hayo zilizoteketezwa 3 ni za kivita
huko mmoja ikiwa ya Kubebea wanajeshi au mizigo ambapo Wanajeshi wa
Kenya walikuwa nayo wakati waliposhambuliwa.
Ndege
4 za Wanajeshi wa Kenya zilishiriki kwenye makabiliano ya leo na
zilisomba miili ya wanajeshi wa Kenya waliouawa na majeruhi ambazo
zilizkuwa zimezagaa kwenye msitu wa pori kwenye eneo la mapigano.
Wafugaji wanasema walisikia milio ya silaha nzito na yale ya rashasha ambazo washambulianaji walikuwa wakirushiana.
Endelea kufuatilia huenda tukawaletea ufafanuzi zaidi kuhusiana na makabiliano hayo ya Kulbiyo.