UFAFANUZI:Magari za Wanajeshi wa Kenya zilizoteketezwa kwenye mapambano ya mji wa Kulbiyow na Ndege zinazosomba maiti za Wanajeshi waliouawa.

Monday June 23, 2014 - 16:59:01
7652
Super Admin
Habari kutoka mikoa ya Lower Jubba zinaeleza kuwa kumekuwa na makabiliano makali yaliodumu masaa kadhaa katika Maeneo ya miji ya Kulibiyow na Badade karibu na mipaka ya kizushi kati ya nchi hizi mbili ya Somalia na Kenya.





Vyanzo vya kuaminika vinaeleza kuwa Mujahidina wa Wilayatul Islamiah ya Lower Jubba walifanya shambulio la kushtukisha dhidi ya Msafara wa Wanajeshi waliokuwa wakitembe eneo la mpaka ambapo mapigano yalidumu takriban masaa matatu mfululizo.






Waandishi wa habari waliopo mkoa wa Jubba wanasema Magari 4 ya Wanajeshi wa Kenya zimeteketezwa na Wanajeshi waliouawa ni zaidi ya Wanajeshi 10.




Habari zaidi zinaeleza kuwa kati ya Magari hayo zilizoteketezwa 3 ni za kivita huko mmoja ikiwa ya Kubebea wanajeshi au mizigo ambapo Wanajeshi wa Kenya walikuwa nayo wakati waliposhambuliwa.






Ndege 4 za Wanajeshi wa Kenya zilishiriki kwenye makabiliano ya leo na zilisomba miili ya wanajeshi wa Kenya waliouawa na majeruhi ambazo zilizkuwa zimezagaa kwenye msitu wa pori kwenye eneo la mapigano.





Wafugaji wanasema walisikia milio ya silaha nzito na yale ya rashasha ambazo washambulianaji walikuwa wakirushiana.






Endelea kufuatilia huenda tukawaletea ufafanuzi zaidi kuhusiana na makabiliano hayo ya Kulbiyo.

Related Items

Update cookies preferences