Askari auawa na kisha Bunduki yake kuchukuliwa katika mji wa Marka.

Wednesday July 16, 2014 - 23:32:34
7757
Super Admin
Habari kutoka mkoa wa Lower Shabelle zinaeleza kuwa mashambulio mapya yamefanyika dhidi ya Wanamgambo wa Serikali shirikisho ya Somalia (FG) inayofanyakazi na maadui waliovamia Ardhi ya Somalia.



Askari mmoja wa Serikali ameuawa na watu waliokuwa wamejihami na Silaha katika Soko la mji wa Marka ambapo Askari huyo wakati anauawa alikuwa akila Miraa.




Walioshudia wanasema baada ya kumwua Askari huyo wauaji walichukua Bunduki yake ya AK47 na kiboksi chake,habari zaidi zinaeleza kuwa Askari mwingine amejeruhiwa katika mtaa wa Rashia.




Ilikuwa siku mmoja tu wakati ilipofanyika shambulio kama hili ndani ya mji wa Marka na itakumbukwa mji huo kuna Wanajeshi wa Kigeni.




Mahad Yare


SomaliMemo,Mugadishu


Related Items

Update cookies preferences