Uturuki yafunga Balozi wake mjini Mugadishu kwa Muda kutokana na hali mbaya ya Usalama.

Tuesday July 15, 2014 - 10:37:22
7373
Super Admin
Huko hali mbaya ya usalama ukiongezeka siku hadi siku mjini Mugadishu Serikali ya Uturuki imetangaza kufunga Ubalozi wake iliopo nchini Somalia.




Taarifa rasmi uliotolewa na na Serikali ya Uturuki ilisema kuwa kutokana na hali mbaya inayoikumba mji mkuu wa Somalia Mugadishu imeamua kuwaruhusu wafanyakazi wake kuondoka kwenye ubalaozi huo hadi hapo Amri nyingine itakapotolewa.





Duru za kuaminika zilieleza kuwa Maofisa wa Kituruki walioko kwenye ofisi hiyo ya Ubalozi wamepelekwa hadi katika upande wa Uwanja wa Ndege wa kimataifa mjini Mugadishu huko Majengo ya Ubalozi huo ukiachiwa Maaskari wachache wa Kisomali kulinda.





Kufungwa kwa ubalozi wa Uturuki unakuja wakati ambapo mji wa Mugadishu ukiwa unashuhudia Mauaji ya kupangwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Banadir.




Uturuki ni sehemu ya Mataifa ya Wavamizi wa Kigeni ambapo sana ulikuwa ukijihusisha upande wa kuharibu maadili ya Dini ya Kislaam kwa jamii ya Wasomali na itakumbukwa Serikali hiyo inatoa ufadhili kwa Uvamizi wa AMISOM nchini Somalia.

Related Items

Update cookies preferences