VIDEO+PICHA:Ndege zisizo na Rubani za Mujahidina wa Falastine yaanza kazi na kushambulia Israel.

Tuesday July 15, 2014 - 23:41:07
14455
Super Admin
Habari kutoka mji wa Ghaza zinaeleza kuwa Wanajeshi wa Kizayuni wa Israel baado wanaendelea na mashambulio yao dhidi ya wananchi wa Falastine.




Mamia ya waislaam wamekwisha pata kuwa Mashuhadaa kwenye mashambulizi hizo za Mayahudi katika mji wa Ghaza.




Pamoja na mauaji hayo kutoka Utawala haramu wa Israel lakini kuna taarifa ya kufurahisha kutoka upande wa Makundi ya Muqawamah wa Falastine ambapo kwa mara ya kwanza wameanza kutumia Ndege za Kijeshi zisozokuwa na Rubani.




Kikosi cha Izzudiin Qasam cha Jeshi la Hamas wametangaza kutumia Ndege 3 za Kijeshi aina ya Drone kwenye makabiliano yake dhidi ya Israel.

http://wata.cc/up/2014/07/images/w-b0423b0afe.jpg

Taarifa iliyotolewa na Izzudiin Qasam ilifafanua Ndege iliyotumiwa na Mujahidina Ndege iliyotajwa kwa jina la AIC ilitumwa kutoka mji wa Ghaza kwa kazi maalum ndani ya Ardhi wanayoikalia kwa Nguvu ya Israel.




Ndege nyingine ya Pili ina jina la AIB yenyewe ni ya Istish-haadiyah na ina uwezo wa kubeba mtu mmoja na ina uwezo wa kufanya mashambulio maeneo maalum yaliopangwa.




Hata hivyo ndege nyingine iliyobeba jina la AIA imeruka hadi kwenye mji wa Telaviv khususan kwenye majengo ya Wizara ya Ulinzi wa Israel ingawa baadae ilitunguliwa.




Dunia imeshangazwa namna wapiganaji Mujahidina wa Falastine walivyoweza kutumia Ndege walizotengeneza wenyewe na Ndege hizo zimepewa jina la "Ababiil".


TIZAMA VIDEO HAPA CHINI



Related Items

Update cookies preferences