Takriban Maaskari 10 wa Serikali ya TFG wauawa kwenye mji wa Afgooye.

Monday June 23, 2014 - 21:05:14
8154
Super Admin
Askari wa Serikali ya TFG aliyeuawa.
Askari wa Serikali ya TFG aliyeuawa.
Takriban Maaskari 10 wa Serikali ya TFG wameuawa kwenye mji wa Afgooye iliyo Mkoa wa Lower Shabelle.





Walioshuhudia wanasema Askari mmoja wa Serikali ya TFG aliwaua mara mmoja Maaskari wenzake 5 na kisha baadae na yeye aliuawa papo hapo na Maaskari wengine waliokuwa kwenye eneo la Beria la kukusanya pesa kwa raia.





Kitendo hicho kilicho leta athari katika mji wa Afgooye imekuja baada ya Maaskari hao 5 waliouawa na Askari huyo mwenzao siku za nyuma kumpokonya Bunduki lake kwa nuguvu na hasira hiyo ilisababisha kuwatwanga Risasi.





Upande mwingine kunaarifiwa mapigano ya kikoo katika Mji wa No.50 iliyo mkoani Lower Shabelle,habari za kuaminika zinaeleza kuwa Makundi mawili ya wanamgambo wamepigana siku ya jana jioni na kusababisha hasara.





Kwenye miji na Vijiji mkoani Lower Shabelle ambayo kuna nidhamu ya Sheria za Kislaam ni baadhi ya maeneo yalio na utulivu na ni marufuku mauaji na uporaji pamoja na ma'siya ya kila aina.




Liban Jehow Abdi



SomaliMemo,Mugadishu



Related Items

Update cookies preferences