Mashambulio mengine mapya katika Kisiwa cha Lamu nchini Kenya na Milipuko yaliofanyika mji wa Wajear.

Tuesday July 08, 2014 - 16:31:36
8072
Super Admin
Nchini Kenya mashambulio yanayolenga Wanajeshi na Maofisa wa Usalama pamoja na Raia wa Kenya waliowatuma vijana wao kuja nchini Somalia bado yamendelea.



Kwa uchache mtu mmoja ameuawa na na wengine kujeruhiwa baada ya kurushwa Bomu katika mgahawa mmoj wa usiku uliopo mji wa Wajear kaskazini mwa Kenya.




Vyanzo muhimu vinaeleza Mgahawa ulioshambuliwa ulikuwa ukimilikiwa na Wakenya Manasara,Maofisa wa Polisi wanasema mtu mmoja ameuawa kwenye tukio hilo na wengine 5 wamejeruhiwa.





Baada ya mlipuko huo watu waliokuwa na silaha walifyatua risasi na kusababisha hasara zaidi kwenye eneo lililoshambuliwa.





Upande mwingine kumefanyika shambulio lingine kwenye kijiji cha Hindi Kisiwani Lamu,Maofisa wa Polisi wamethibitisha kutokea tukio hilo lakini hawakufafanua hasara iliyopataikana kwenye shambulio hilo.





Msemaji aliyezungumza kwa niaba ya Harakat Al-Shabab Al Mujahideen amesema shambulio hilo limefanywa na vikosi vyao na Kenya wametwishwa hasara kubwa.




Ndani ya wiki mmoja Kenya imeshuhudia misururu ya mashambulio yaliofanyika ndani mwa nchi yake ambapo yamegharimu maisha ya zaidi ya Wakenya 40 na mashambulio yote yamethibitishwa kuhusika na Al-Shabab.





Serikali ya Kenya imetumia nguvu ya Kijeshi kuingia Mikoa ya Kusini ya Jubba na Gedo na Mujahidina nao wameingia kwa Nguvu ndani ya Ardhi ya Kenya na kutekeleza Kisasi juu ya wahusikao mauaji yaliofanyika Somalia.





Liban Jehew Abdi


SomaliMemo,Mugadishu


Related Items

Update cookies preferences