Shambulio jingine iliyosababisha hasara yafanyika kisiwa cha LAMU nchini Kenya.

Friday July 11, 2014 - 23:04:01
8363
Super Admin
Habari kutoka nchini Kenya zinaeleza kuwa kumefanyika mashambulio mengine ndani ya Ardhi ya Kenya wakati ambapo hali ya usalama katika nchi hiyo ukiyumba vibaya.





Habari kutoka kwenye Kisiwa cha kitalii cha mji wa Lamu zinaeleza kuwa watu waliojihami na silaha jana usiku walifanya shambulio iliyolenga baadhi ya maeneo yaliopangwa kushambuliwa ndani ya mji huo.




Karisa Charo ambae ni mtaalamu mkazi wa Lamu amewaambia vyombo vya habari ndani ya Kenya kuwa Washambuliaji jana walichomo Maeneo ya Biashara na Majumba kadhaa kwenye kisiwa hicho.





Afisa wa Usalama wa Serikali ya Kenya ambae alizungumza na vyombo vya habari amesema Washambuliaji wapatao 300 walishambulia mji wa Lamu na kuchukua Silaha za Maaskari wa Polisi zilizokuwepo kwenye kituo cha Polisi wa Lamu.





Serikali ya Kenya tangu kupeleka Wanajeshi wake nchini Somalia mwaka 2010 imekumbwa hali ya ukosefu wa Usalama na mamia ya Wanachi na Maofisa wa Serikali pamoja na Wanajeshi wa Kenya wakiuawa.



Mahad Yare


SomaliMemo,Mugadishu


Related Items

Update cookies preferences