Maaskari waliouawa kwenye mji wa Afgooye na shambulio iliyofanyika mji wa Yaqshiid.

Thursday June 12, 2014 - 11:14:56
11633
Super Admin
Habari kutoka Wilaya ya Afgooye mkoani Lower Shabelle zinaeleza kuwa kumefanyika shambulio kwenye basi waliokuwa wakisafiri Wanajeshi wa Serikali ya TFG na kusababisha hasara.
Usiku wa kuamkia leo watu wasiofahamika walishambulia kwa bomu la kurushwa mkono Basi hilo na kusababisha vifo vya Maaskari 3 na wegine 5 kujeruhiwa viabaya kwenye shambulio hilo.

Gari waliokuwemo Maaskari wa Serikali ya TFG iliharibiwa vibaya kutokana na shambulio hilo,maofisa wa Serikali kwenye Wilaya ya Afgooye wamesema wameanza msako wa kuwaska washambuliaji waliofanya shambulio hilo.

Upnade mwingine jana usiku watu waliokuwa wamejihami na silaha walishambulia kambi la Jeshi la TFG kwenye kituo cha Televisheni cha zamani iliyopo mtaa wa Tawfiiq Wilayani Yaqshiid.

Liban Jehow Abdi
SomaliMemo,Mugadishu

Related Items

Update cookies preferences